Sephora Nyomi: Hali ya afya ya akili iko kwa shida Ituri
Matatizo yanayosababisha vurugu za kiakili yameongezeka kwa kiasi kikubwa katika kipindi cha miaka miwili iliyopita katika jimbo la Ituri, ambalo linakumbwa na harakati za makundi yenye silaha. Haya ni angalizo lililotolewa na Mpango wa Taifa wa Afya ya Akili wakati maadhimisho ya awali ya Siku ya Afya ya Akili Duniani.